• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mbeya City Council
Mbeya City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Tehama
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
    • Orodha ya Wah Madiwani
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

MADIWANI JIJI LA MBEYA WAPITISHA MPANGO WA BAJETI 2021/2022

Imewekwa Tarehe: February 19th, 2021

Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya wapitisha kiasi cha Shilingi 74,964,752,348/= kama Makadirio ya Mapato na Matumizi ya mpango wa Bajeti ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Akiwasilisha makadirio hayo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya Bwana Amede E.A, Ng’wanidako amesema Halmashauri imepanga kukusanya kiasi cha Shilingi 74,964,752,348/= huku fedha hizo zikigawanyika kutokana na vyanzo mbalimbali ikiwemo kiasi cha shilingi 16,645,537,804/= ambacho kitakusanywa kutokana na mapato ya ndani, Shilingi 1,642,881,000/= ikiwa ni ruzuku kutoka serikali kuu (OC), shilingi 49,002,520,000/= sehemu ya ruzuku kutoka serikali kuu itakayohusika na mishahara ya watumishi, Shilingi 3,581,811,044/= kwaajili ya miradi ya maendeleo.

Huku Shilingi 2,892,002,500/= zikiwa ni fedha za Elimu bila Malipo na Shilingi 1,200,000,000/= zikitarajiwa kuwa michango ya wananchi katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Aidha Amede amesema katika kipindi cha 2021/2022 Halmashauri imekusudia kutumia jumla ya Shilingi 74,964,752,348/= kati ya hizo , vyanzo vyake vya ndani ni shilingi 16,645,537,804/=, Ruzuku ya mishahara shilingi 49,002,520,000/=, Matumizi ya kawaida Shilingi 1,642,881,000/=, Miradi ya maendeleo  ni Shilingi 3,581,811,044/=, Elimu bila malipo Shilingi 2,892,002,500/= huku michango ya wananchi ikikadiriwa kufikia kiasi cha shilingi 1,200,000,000/=

Akiendelea na maelezo yake Mkurugenzi Amede amesema Jiji la Mbeya limekisia kukusanya Shilingi 16,645,537,804/= kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato ya ndani ya Halmashauri , huku makisio hayo yakiongezeka kutoka Shilingi 15,949,288,000/= kwa mwaka wa fedha 2020/2021, ongezeko hilo linatokana na Mapato yatokanayo na mauzo ya viwanja na makusanyo yatokanayo na Ada za wanafunzi wa shule ya mchepuo wa kiingereza inayojengwa katiak Kata ya Nsalaga, aidha kiasi cha shilingi 7,304,232,580 sawa na 69.4% ya mapato yasiyolindwa kimetengwa kwaajili ya miradi ya maendeleo.

Kwa upande wa vipaumbele Halmashauri ya Jiji la Mbeya imepanga kuboresha miundombinu ya Elimu msingi kwa kujenga idadi ya madarasa 52, kutengeneza madawati 900 na matundu ya vyoo 52, kuboresha miundombinu ya Elimu sekondari kwa kujenga madarasa 50, madawati 1,250 na matundu ya vyoo 54, Kujenga vituo vitatu vya afya, Kujenga kitega uchumi cha Hostel ya kupangisha wanafunzi wa vyuo, Kulipa madeni ya wazabuni, Kuongeza mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kuboresha mifumo ya kukusanyia mapato.

Mara baada ya wasilisho hilo la Mkurugenzi ndipo Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya Dormohamed Issa Rahmat alipo wauliza wajumbe kama wanakubaliana na wasilisho hilo la Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya. Wajumbe hao wote kwa pamoja waliafiki Makadirio hayo kuwa mpango wa Bajeti ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Matangazo

  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 JIJI LA MBEYA December 18, 2020
  • JOINING INSTRUCTION YA SHULE ZA SEKONDARI KWA WANAFUNZI WATARAJIWA WA KIDATO CHA KWANZA December 16, 2020
  • SHERIA ZINAZOSUBIRI UIDHINISHAJI WA TAMISEMI July 21, 2020
  • TAARIFA YA MREJESHO CITY PARK April 03, 2020
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SHILINGI 269,501,500.00 ZATOLEWA NA JIJI LA MBEYA KWA MAKUNDI YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

    March 12, 2021
  • MADIWANI JIJI LA MBEYA WAPITISHA MPANGO WA BAJETI 2021/2022

    February 19, 2021
  • WAKAZI WA MWANSEKWA MBIONI KUPIMIWA ARDHI YAO

    February 15, 2021
  • MADIWANI JIJI LA MBEYA WAJITOKEZA KUFANYA USAFI

    January 30, 2021
  • Tazama Zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

"MSITUBIPU KATIKA UCHAGUZI " RC MBEYA
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Mbeya City Football Club
  • Google
  • Halmashauri ya Jiji la Mbeya Ukurasa Maalumu

Tovuti Mashughuli

  • Poralg Website
  • Ikulu Website
  • Public Service Website
  • Tanzania Website
  • eGA
  • Secretariati ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mbalizi Road near TTCL Offices

    Anuani ya Posta: 149 Mbeya

    Simu: +25525252502372

    Simu ya Kiganjani: +255 25 2502563

    Barua Pepe: cd@mbeyacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbeya City Council . All rights reserved.