• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mbeya City Council
Mbeya City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Tehama
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
    • Orodha ya Wah Madiwani
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

MADIWANI WARIDHIA KULIGAWA JIJI LA MBEYA

Imewekwa Tarehe: January 29th, 2021

Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya wameridhia kwa pamoja mchakato wa uanzishwaji wa Halmashauri mpya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya, ridhaa hiyo imetolewa katika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya ulioketi siku ya tarehe 29/01/2021 katika ukumbi wa Mikutano wa Jiji la Mbeya wa Mkapa.

Akiwasilisha taarifa ya Kamati Maalumu ya uanzishwaji wa Halmashauri mpya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya iliyoundwa na Kamati ya fedha na Utawala ya Halmashauri hiyo, Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya ndugu Amede E.A, Ng’wanidako aliwaeleza wajumbe wa Mkutano wa Baraza kuwa taratibu za uanzishwaji wa Halmashuri mpya ndani ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa zipo kwa mujibu wa ibara ya 145 (1) na 146 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1997 na sheria namba 8 ya serikali za mitaa za mwaka 1984 sura 288.

Mkurugenzi Amede aliendelea kueleza kuwa hatua za uanzishwaji wa Mamlaka za serikali za Mitaa zimeanishwa katika mwongozo wa uanzishwaji serikali za Mitaa za mwaka 2014 uliotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Mwongozo huo umefafanua zaidi utaratibu wa kuanzisha Mamlaka ya Mji au kupandisha hadhi maeneo ya Utawala.

Aidha ndugu Amede alisema kwamba wajumbe walioteuliwa katika Kamati hiyo ni pamoja na Mheshimiwa Daudi Ngogo- Mwenyekiti, Mheshimiwa Dormohamed Issa Rahmat – Mjumbe, Mheshimiwa Agness Mangasila – Mjumbe, Mheshimiwa Daktari Tulia Ackson – Mjumbe, Mheshimiwa Ibrahim Mwampani- Mjumbe, Mheshimiwa Daniel Mwaibindi – Mjumbe, Mheshimiwa Adam Simbaya – Mjumbe pamoja na wataalamu ambao ni

Ndugu Amede E.A, Ng’wanidako, Mashaka Semkiwa, Dickley Nyato, Triphonia Kisiga, Oscar Kapinga , Adon Hajayand na Gerald Ruzika.

Majina ya waliopendekezwa katika kamati hiyo ni majina ya Madiwani kutoka Kamati ya Fedha na utawala ambao ni Mstahiki Meya , Naibu Meya na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini kwa nafasi zao, wengine ni wenyeviti wa Kamati za Mipangomiji na Ardhi na Kamati ya Uchumi ,Afya na Elimu na wajumbe wawili wa kuteuliwa ambao wanatoka kila kamati kwa kuzingatia uwakilishi wa Tarafa mbili za Iyunga na Sisimba.

Mchakato huu wa uanzishwaji wa Halmashauri mpya ndani ya Jiji la Mbeya unatokana na ahadi iliyotolewa katika ziara za kampeni na Mgombea wa kiti cha Rais kupitia Chama cha Mapinduzi ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Daktari John Pombe Magufuli mnamo tarehe 30, Septemba, 2020 na kusisitiza kuwa iwapo atachaguliwa kuwa Rais ataligawa Jiji la Mbeya na kuwa na Halmashauri mbili na kuagiza kikao cha kwanza cha Baraza pamoja na mambo mengine kijadiri mchakato wa uanzishwaji wa Halmashauri mpya.

Matangazo

  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 JIJI LA MBEYA December 18, 2020
  • JOINING INSTRUCTION YA SHULE ZA SEKONDARI KWA WANAFUNZI WATARAJIWA WA KIDATO CHA KWANZA December 16, 2020
  • SHERIA ZINAZOSUBIRI UIDHINISHAJI WA TAMISEMI July 21, 2020
  • TAARIFA YA MREJESHO CITY PARK April 03, 2020
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SHILINGI 269,501,500.00 ZATOLEWA NA JIJI LA MBEYA KWA MAKUNDI YA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

    March 12, 2021
  • MADIWANI JIJI LA MBEYA WAPITISHA MPANGO WA BAJETI 2021/2022

    February 19, 2021
  • WAKAZI WA MWANSEKWA MBIONI KUPIMIWA ARDHI YAO

    February 15, 2021
  • MADIWANI JIJI LA MBEYA WAJITOKEZA KUFANYA USAFI

    January 30, 2021
  • Tazama Zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

"MSITUBIPU KATIKA UCHAGUZI " RC MBEYA
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Mbeya City Football Club
  • Google
  • Halmashauri ya Jiji la Mbeya Ukurasa Maalumu

Tovuti Mashughuli

  • Poralg Website
  • Ikulu Website
  • Public Service Website
  • Tanzania Website
  • eGA
  • Secretariati ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mbalizi Road near TTCL Offices

    Anuani ya Posta: 149 Mbeya

    Simu: +25525252502372

    Simu ya Kiganjani: +255 25 2502563

    Barua Pepe: cd@mbeyacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbeya City Council . All rights reserved.