• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mbeya City Council
Mbeya City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Tehama
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
    • Orodha ya Wah Madiwani
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

JIJI LA MBEYA LAAHIDI KUPAMBANA NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA KWA WATUMISHI WAKE

Imewekwa Tarehe: March 8th, 2022

Halmashauri ya Jiji la Mbeya imeadhimisha siku ya Wanawake Dunia kwa kutangaza kupambana na unyanyasaji wa kijinsia kwa watumishi ambao watakwenda kinyume na haki za mwanamke na binadamu kiujumla.

Akiongea kwenye hafla ya maadhimisho hayo yaliofanyika kwenye ukumbi wa Mkapa Jijini Mbeya Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya Bi.Agnes Mangasila amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa utendaji kazi wake na kuwataka wanawake watumishi wasimuangushe, watende kazi ipasavyo kama ambavyo mkuu huyo wa nchi anavyopambana kuleta maendeleo.

Aidha Naibu Meya Mangasila amefafanua kuwa Mkoa na Jiji la Mbeya limekuwa na bahati mwaka huu kwa kumpata kiongozi mkuu wa moja ya mihili mitatu ya nchi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Tulia Ackson ambaye ni mwanamke mpigania maendeleo bila kujali yanakwenda upande gani wa nchi hivyo amewataka wanawake waendelee kuamka kupambania haki na maendeleo.

Kwa upande wake mwakilishi wa Mkurugenzi wa Jiji Bi.Upendo Haule ambaye pia ni Mkuu wa idara ya Utawala na Utumishi amesema hatakuwa tayari kuona unafanyika unyanyasaji wowote wa kijinsia kwenye Halmashauri Jiji la Mbeya ambayo yeye anaisimamia katika sekta ya utumishi na utawala .

Bi. Upendo Haule amewataka wale wote watakaopatwa na kadhia ya unyanyasaji wa kijinsia wasisite kutoa taarifa ili hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi ya wanaofanya tabia hiyo inayopingwa Duniani na mbinguni.

“Mimi ndiye ninayesimamia nidhamu ya watumishi naomba mwanamke yeyote ambaye atafanyiwa kitendo cha unyanyasaji kazini atoe taarifa kwenye ofisi yangu hakuna atakayesalimika kwa mujibu wa sheria “amesema Bi.Upendo Haule Mkuu wa idara ya Utawala na Utumishi wa Jiji la Mbeya.

Sherehe ya siku ya Wanawake hufanyika Duniani kote kila mwaka ifikapo Machi 8 ambapo kwa Tanzania mwaka huu kitaifa imefanyika Unguja Visiwani Zanzibar huku mgeni rasmi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan zikiwa na kauli mbiu Kizazi cha haki na usawa kwa maendeleo endelevu .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI May 25, 2022
  • TANGAZO LA MNADA May 10, 2022
  • TANGAZO LA KUHAIRISHA MNADA WA HADHARA LILILOTOLEWA NA HALMASHAURI YA JIJI LA MBEYA April 25, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA April 21, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • JIJI LA MBEYA LAUZA MALI ZAKE CHAKAVU

    May 26, 2022
  • ALAT YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI JIJI LA MBEYA

    April 20, 2022
  • TCI YATOA MAFUNZO KWA MADIWANI JUU YA ELIMU YA AFYA YA UZAZI KWA VIJANA

    April 19, 2022
  • CCM YARIDHISHWA NA MIRADI YA MBEYA JIJI

    March 18, 2022
  • Tazama Zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

"MSITUBIPU KATIKA UCHAGUZI " RC MBEYA
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Mbeya City Football Club
  • Google
  • Halmashauri ya Jiji la Mbeya Ukurasa Maalumu

Tovuti Mashughuli

  • Poralg Website
  • Ikulu Website
  • Public Service Website
  • Tanzania Website
  • eGA
  • Secretariati ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mbalizi Road near TTCL Offices

    Anuani ya Posta: 149 Mbeya

    Simu: +25525252502372

    Simu ya Kiganjani: +255 25 2502563

    Barua Pepe: cd@mbeyacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbeya City Council . All rights reserved.