• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Mbeya City Council
Mbeya City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Tasisi
    • Idara
      • Afya
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utumishi na Utawala
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi
      • Mipango na Uchumi
      • Fedha na Biashara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Tehama
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Mipangomiji na Mazingira
      • Kamati ya Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wah Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
    • Orodha ya Wah Madiwani
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

JIJI LA MBEYA LATOA SHILINGI MILIONI 200 ZA MAPATO YAKE YA NDANI UJENZI WA KITUO CHA AFYA ILEMI

Imewekwa Tarehe: September 22nd, 2021

Halmashauri ya Jiji la Mbeya imetoa kiasi cha Shilingi Milioni 200 ya Mapato yake ya ndani ujenzi wa kituo cha Afya Kata ya Ilemi Mtaa wa Masewe ambacho kwa awamu ya kwanza na ya pili kinatarajiwa kugharimu kiasi cha Shilingi 524,660,215.50.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya Ndugu Amede E.A, Ng’wanidako amesema kiasi hicho cha fedha tayari kimeshawekwa kwenye akaunti ya Kata ya Ilemi tayari kwa ujenzi wa kituo hicho, na kubainisha kuwa fedha hizo ni sehemu ya mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya na kuwahakikishia wananchi wa Kata hiyo kuwapekekea fedha zaidi ili kukamilisha ujenzi huo kwa wakati.

Nae Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya katika hotuba yake alieleza mipango ya serikali ni kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi wake na ndio maana Halmashauri ya Jiji la Mbeya imetoa kiasi hicho cha fedha na itaendelea kutoa ili huduma ziwe karibu na wananchi.

Kaimu katibu tawala wa Wilaya ya Mbeya ndugu Vincent Mbua kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mbeya amewasihi wananchi hao kushirikiana katika ujenzi huo ili kukamilisha kwa wakati na kuwaomba wananchi hao kuwa walinzi wa mradi huo ili usiingie doa kwa matukio yasiyo na tija kama wizi na upotevu wa mali za mradi huo.

Akizindua ujenzi wa kituo hicho Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewasihi wananchi wa Kata hiyo kujitolea katika ujenzi wa kituo hicho cha Afya kwani ni mali yao “Ndugu zangu kituo hiki ni mali yetu sote hivyo kila mwananchi anawajibu wa kuchangia ujenzi wa kituo hiki kwani kitasaidia kutoa huduma ndani ya Kata yetu pamoja na Kata jirani “ alisema Dkt Tulia.

Aidha Dkt Tulia aliongoza Harambee na kufanikisha kupatikana kwa mifuko 274 ya Saruji huku Ofisi yake ikichangia mifuko 100 ya saruji na kutanabaisha kuwa mifuko hiyo ya saruji itapelekwa eneo la ujenzi ili kusaidia ujenzi wa kituo hicho, huku akiwataka waliotoa ahadi katika harambee hiyo kukamilisha ahadi zao ndani ya miezi mitatu

Katika ujenzi huo wa kituo cha afya wananchi wao wamejitolea nguvu kazi kwenye kuchimba msingi na shughuli nyingine zinazohusu ujenzi huo ikiwemo ung’oaji wa visiki pamoja na kusawazisha eneo la mradi

Ujenzi wa kituo hicho unataraijiwa kukamilika ndani ya miezi sita ili huduma zianze kutolewa kwa wananchi.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI May 25, 2022
  • TANGAZO LA MNADA May 10, 2022
  • TANGAZO LA KUHAIRISHA MNADA WA HADHARA LILILOTOLEWA NA HALMASHAURI YA JIJI LA MBEYA April 25, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA April 21, 2022
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • JIJI LA MBEYA LAUZA MALI ZAKE CHAKAVU

    May 26, 2022
  • ALAT YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI JIJI LA MBEYA

    April 20, 2022
  • TCI YATOA MAFUNZO KWA MADIWANI JUU YA ELIMU YA AFYA YA UZAZI KWA VIJANA

    April 19, 2022
  • CCM YARIDHISHWA NA MIRADI YA MBEYA JIJI

    March 18, 2022
  • Tazama Zote

Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa

"MSITUBIPU KATIKA UCHAGUZI " RC MBEYA
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Mbeya City Football Club
  • Google
  • Halmashauri ya Jiji la Mbeya Ukurasa Maalumu

Tovuti Mashughuli

  • Poralg Website
  • Ikulu Website
  • Public Service Website
  • Tanzania Website
  • eGA
  • Secretariati ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watu waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Mbalizi Road near TTCL Offices

    Anuani ya Posta: 149 Mbeya

    Simu: +25525252502372

    Simu ya Kiganjani: +255 25 2502563

    Barua Pepe: cd@mbeyacc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2018 Mbeya City Council . All rights reserved.